Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Saturday, July 13, 2013

HAYA NDIO MAJIBU YA DR SLAA JUU YA UZUSHI WA MWIGULU NCHEMBA KUHUSU RED BRIGED

Jitihada za Mwigulu kuhusianisha Red Brigade ya CHADEMA na Brigate Rosse ( neno la ki Italiano. Lenye maana ya Red Bigades) ni propaganda ya Kipuuzi. Red Brigade ( inaitwa brigedi Nyenyekundu) ya CHADEMA, ambayo ipo kwa mujibu wa Katiba ya Chadema na Kanuni zetu. Fasili na Ufafanuzi wa Brigedi Nyekundu ni "..Chombo cha ulinzi na usalama wa mali na maslahi ya Chama na viongozi"( Rejea Kanuni za Uendeshaji Kazi za Chama... kif. B " Fasili na Ufafanuzi". Wajibu wa kujilinda ni wa kila mtu na chama nacho kina wajibu wa kulinda Mali zake, wanachama wake na viongozi wake.

Aidha Mwigulu anazungumzia "Brigate Rosse". Ni dhahiri Mwigulu anafanya siasa ya maji Taka. Kwanza ni vema Mwigulu wajulishe wasomaji Kama neno hilo Lina maana ile ile ya "Red Brigade", na je Red Brigade ya CHADEMA in a fasili na Tafsiri ile ile ya CHADEMA? Kama ndivyo atuwekee Katiba ya Brigate Rosse hadharani ili wanaJF na GT wote wafanye uchambuzi wa kina na kuona Kama anachosema Mwigulu ni sahihi au ni Propaganda tu!

Ni kweli Dr. Slaa nimesoma Roma Italia toka 1979 hadi 1981. Hivyo siyo tu ninajua na kuzungumza Kiitalia, lakini pia ninafahamu Brigate Rosse ya Italia kwa kuwa miaka hiyo ndio kipindi kulikuwa na umafia na uhalifu mkubwa na kulikuwa na kesi denying dhidi ya Mafia. Katika Masomo yangu ya Sheria,kesi hizo Mara nyingi zimekuwa rejea ya Maprofesa. Hivyo ninaijua si kwa kuwa nimeishi katika utamaduni wa Italia wa wakati huo.

Hata hivyo, Ndio maana sikuzote, Sina sababu ya kujibu upuuzi wa Mwigulu. serikali iliyoko madarakani ni ya CCM. Kama ni kweli anayosema Mwigulu na anayaamini, Anashangaza sana. Dr. slas nimemaliza masomo yangu mwaka 1981. Tangu wakati huo sijarudi Roma isipokuwa kipindi nilipokuwa Katibu Mkuu wa TEC. Sasa Mwigulu anataka kusema TEC nayo ilikuwa inanzisha Brigate Rosse kwa kuwa Kama Katibu wajibu wangu ulikuwa kuunganisha Baraza letu na Nchi zingine duniani.kauli ya Mwigulu,unaweza kutolewa tu na mtoto wa darasa la pili.

Aidha, Kama Anachosema Mwigulu ni kweli anapaswa kukamatwa,kwani Kama Raia Mwema, toka mwaka 1981 Mwigulu alikuwa na Taarifa ya mtu aliyejifunza mbinu za Brigate Rosse, ambazo ni makundi ya uhalifu na Umafia na Mwigulu amekaa na Taarifa hizo za kihalifu na kwa kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, mwenye kukaa na Taarifu za uhalifu na yeye ni mhalifu. Anapaswa akamatwe kwa ushiriki wake kwenye uhalifu huo. Katika Hali ya kawaida sina hakika Kama Mwigulu aliwahi kujifunza kitu kinachoitwa logic katika maisha yake. Kuelewa kuwa Kaulinzako zinajikanyaga huhitaji sana kwenda shule kubwa kubwa, unless mnatuambia Chuo Kikuu kilichompa Degree ni hovyo kiasi hicho. Kwa maana nyingine, Kama kweli Mwigulu ni Naibu Katibu Mkuu, Serikali aliyoko ni hiyo hiyo ya CCM toka miaka 1977, maana yake ni kuwa Serikali hiyo ambayo inamjua mhalifu muda wote tcoka 1981, inaibuka Leo na kauli tata hivi, wakati Katiba ya CHADEMA ipo kwa Msajili toka mwaka 2006 basi wakubali Serikali ya CCM imeshindwa kuongoza na ilipaswa kujiuzulu siku nyingi sana.

Nadhani nimejieleza ya kutosha. Nawaomba wasomaji wetu wapuuze upuuzi huu wa Mwigulu nchemba
BY DR SLAA

No comments:

Post a Comment