Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema jana kwamba pamoja na hatua yake
ya kutoroka, jeshi litaendelea kumsaka kwa udi na uvumba ilikumhoji na kujiridhisha kama
kweli ni mwanajeshi wake kabla ya kumchukulia hatua zakinidhamu kwa mujibu wa
Kifungu cha 147 cha Katiba ya Jamhuri wa Muungano waTanzania ya 1977.
“Huyu kijana inasemekana alishawahi kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), lakini wakati
tunaendelea na uchunguzi alitoroka katika nyumba aliyokuwa amepanga bila ya
taarifa kwa baba mwenye nyumba,” alisema Kanali Mgawena kuongeza.
“Askari huyo alikuwa anaishi katika nyumba ya kupanga mita chache karibu na Kituo cha Polisi
cha Simanjiro, Arusha na alikuwa akijishirikisha na ulinzi shirikishi.”
Alipoulizwa jina la askari huyo,Kanali Mgawe alijibu: “Yeye alikuwa anafahamika mtaani
hapo kwa jina la kamanda.” Hata hivyo, Kanali Mgawe alisema jeshi hilo litahakikisha linatoa
ripoti kamili kwa umma baada ya kumkamata na uchunguzi kukamilika ili kuondoa utata
uliogubika suala hilo.
Alipoulizwa kama kuna tofauti gani kati ya
mwanajeshi kuingia
kwenye mikutano ya wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kisiasa kama wakuu wa wilaya
na mikoa, Kanali Mgawe alijibu:” Wanajeshi wanaofanya kazi za U- DC au RC, wanaruhusiwa
kisheria.”Alifafanua kuwa iwapo mwanajeshi atateuliwa kufanyakazi katika taasisi yeyote ya
Serikali nje ya jeshi, atatakiwa kuvua magwanda ya jeshi na kufanya kazi hiyo mpaka
atakapomaliza muda wake na baada ya hapo ataruhusiwa kurejea jeshini.
kwenye mikutano ya wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kisiasa kama wakuu wa wilaya
na mikoa, Kanali Mgawe alijibu:” Wanajeshi wanaofanya kazi za U- DC au RC, wanaruhusiwa
kisheria.”Alifafanua kuwa iwapo mwanajeshi atateuliwa kufanyakazi katika taasisi yeyote ya
Serikali nje ya jeshi, atatakiwa kuvua magwanda ya jeshi na kufanya kazi hiyo mpaka
atakapomaliza muda wake na baada ya hapo ataruhusiwa kurejea jeshini.
“Kuna kitu kinaitwa ‘secondment.’ Mwanajeshi anaruhusiwa kufanya shughuli
zozote nje ya jeshi iwapo atahitajika kufanya hivyo. Ila kwa masharti ya kuvua magwanda,
hivyo wananchi wasishangae kuwaona baadhi ya askari wetu ni wakuu wa wilaya na mikoa na
baadaye kurudi jeshini kuendelea na majukumu yao,” alisema Kanali Mgawe na
kuongeza: “Askari akiwa katika majukumu yake mapya, atafanya kazi zote
atakazopewa zikiwamo za kisiasa kama ilivyo kwa wakuu wa wilaya na mikoa, lakini
akirudi jeshini, anarudi kuwa askari mwenye utii na kufuata kanuni za jeshi zisizofungamana
na siasa.”
(Chanzo gazeti la
Mwananchi)
No comments:
Post a Comment