Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Thursday, December 20, 2012

MASHINDANO YA MSIGWA CUP YAENDELEA

Leo ni takribani wiki mbili tangu kuanza kwa mashindano ya kombe la Mbunge wa iringa mjini Mch Peter Msigwa yanayoendelea katika viwanja mbalimbali hapa manispaa ya iringa mjini

Kutokana na majukumu mengine kitaifa(ikizingatiwa kuwa yeye ni waziri kivuli wa mali asili na utalii) alishindwa kuwa nao kwa kipindi cha wiki nzima tangu kuanza kwa mashindano hayo.

baada ya mhe kurudi jimboni alianza kutembelea viwanja mbalimbali vya michezo kwa ajili ya kuwapa hamasa na kuwatia moyo wachezaji wao

leo Mhe alitembelea viwanja vya michezo kadhaa katika manispaa na ameshangaa kuona namna vijana walivyoyapokea kwa furaha mashindano hayo



Mhe Peter Msigwa akiwapa mawaidha wachezaji wa "ac milan" na" dabaga road" katika viwanja vya kanisani kata ya ruaha kabla hawajaingia kwenye mchuano


".ac milan" na "dabaga road" wakichuana vikali uwanjani

watoto na vijana waliojitokeza wakifuatilia mpira kwa makini


timu ya ac milan ikiwa katika mapumziko baada ya dakika 45 za awali kukatika huku wakiwa na sare ya kutokufungana

Mhe Peter Msigwa akiwa katika  pozi na wachezaji wa ac milan(wamevaa sare nyeupe) pamoja na dabaga road(wamevaa sare nyeusi) katika viwanja vya kanisani kata ya ruaha




Mhe Msigwa akifuatilia  kwa makini mpira uliokuwa ukichezwa kati ya ac milan na dabaga road


Mpira mlimalizika kwa ac milan kuinyuka timu ya dabaga road magoli 3-1
Hii bado ni  raundi ya kwanza ya michuano hiyo ambayo itafuatiwa na mechi za mtoano

No comments:

Post a Comment