Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Monday, January 21, 2013

WANAFUNZI VYUO VIKUU WAENDELEA KUTOA ELIMU YA URAIA MKOANI IRINGA

Wanafunzi wa chuo kikuu cha RUCO kilichopo mkoani Iringa wanaendelea na mpango wao wa kutoa elimu ya uraia kwa wakazi wa mkoa huo ikiwa ni moja ya majukumu waliyojiwekea.Walianza kwenye jimbo la Iringa mjini(kwa Mhe Peter Msigwa) na sasa wameanza kuzungukia mkoa mzima wa Iringa.


Jana wanafunzi hao walikuwa katika jimbo la Kilolo (kwa Profesa Msolla) katika kijiji cha Lundamatwe.


Kero kubwa inayowakumba wanakijiji hao ni uporwaji wa ardhi zao unaosimamiwa na mwenyekiti pamoja na mtendaji wa kijiji hicho,wajane wamekuwa ndio waathirika wakubwa wa tatizo hilo kwani itokeapo wamefiwa na waume zao basi hunyang'anywa ardhi na wakitaka kudai hupigwa na kutishiwa kupelekwa mahakamani.


Wanafunzi walipata kazi kubwa ya kuwaelimisha wananchi hao juu ya sheria ya ardhi ambayo inaonekana kutokujulikana kabisa kwao,pia waliwataka wananchi hao kuzifahamu haki zao za msingi katika jamii ikiwa ni pamoja na kudai kujua mapato na matumizi ya fedha zao kila ifikapo kipindi cha miezi mitatu

Mafanikio ya mkutano huo yalikuwa ni makubwa kwani baada ya elimu ile kuna wazee walijitokeza na kurudisha kadi za CCM kwa madai kuwa hawakujua namna ambavyo wamekuwa wakinyanyaswa na kuonewa na watawala hao

MATUKIO KATIKA PICHA




Mwenyekiti wa tawi Rose Mayemba akitutubia wananchi wa kijiji cha Lundamatwe



Katibu wa tawi Nicolaus Francis akiwahutubia wananchi


Kamanda Frank Malata akihutubia wananchi wa kijij cha Lundamatwe

Kamanda Gody Maganga akihutubia wananchi wa kijiji cha Lundamatwe



Makamanda wakiwa  katika pozi  kijiji cha Lundamatwe




Kada  mkongwe wa CCM akitoa sababu za kukihama chama hicho

No comments:

Post a Comment