Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Friday, December 28, 2012

BAADHI YA WANASHERIA WATOFAUTIANA JUU YA HUKUMU YA LEMA

Baada ya mahakama kumrudishia ubunge Mh. Godbless Lema ambaye ni mbunge wa Arusha mjini  siku chache zilizopita, baadhi ya wanasheria wametofautiana juu ya hukumu hiyo.

Mwanazuoni aliyebobea katika sheria  na mwenyekiti wa chama cha wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law society), Profesa Issa Shivji pamoja na wanasheria wengine wamesema kuwa sehemu ya hukumu ya lema haikuwa sahihi.

Habari kutoka kwenye moja ya mitandao ya kijamii zinasema mwanazuoni huyo anaishangaa mahakama  kwa kuwanyima  wapiga kura haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi. Pia amesema mahakama haikusimamia sheria bali ilitunga sheria ya kwake kinyume na ile iliyopo.

Lakini wakili wa Lema (Kimomogoro) amepingana na kauli mwanasheria huyo kwa kusema kuwa pengine hakupata nafasi ya kuipitia hukumu kwa umakini.






No comments:

Post a Comment