Aliyewahi kuwa Mwanachama wa CHADEMA na Mgombea ubunge wa Jimbo la Kibaha Habib Mchange anashikiliwa na kituo cha Polisi Mabatini Kijitonyama kwa tuhuma za wizi wa Simu.
Habib Mchange alikamatwa jana usiku na mpaka leo asubuhi alikuwa bado hajapata dhamana. Huku mahojiano yakiwa yanaendelea kituoni hapo.
Habib Mchange alifukuzwa Uanachama wa Bavicha mapema mwezi huu kwa utovu wa nidhamu na usaliti dhidi ya Chadema ambapo mbali na kufukuzwa Bavicha alipoteza pia uanachama wa Chadema kikatiba.
source-jf
No comments:
Post a Comment