Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Sunday, January 6, 2013

KIKWETE AWASHANGAZA WANANCHI,NI KATIKA MAHUDHURIO YAKE MISIBANI


 
Katika hali ya kushangaza imeonekana kuwa Rais wa nchi Jakaya Kikwete amekuwa akihudhuria zaidi misiba ya wasanii nchini lakini si misiba ya watu ambao ni msaada mkubwa kwa taifa hili.
Ukweli ni kwamba kama aliamua kuwa baba mbona amewabagua watoto  namna ya kuwalea na kuwatunza?mbona ni watumishi wengi wa umma wamekufa tena wengine katika vifo vibaya na vya udhalilishaji lakini hatukuona mchango wake?
Hebu angalia matukio haya;
Msiba wa Mwangosi wala salamu za rambirambi hatukusikia!
Amefariki Dkt. Sayi na Prof. Carneiro wote hawa ndio waliokuwa madakatari bingwa pekee wa upasuaji wa watoto pale Muhimbili, hatukusikia Rais kahudhuria.
Mwaka 2009 alifariki Profesa Aziz, Daktari bingwa wa upasuaji pale Muhimbili na aliyetibu watu wengi sana, aliugua na Serikali ilimwambia hawawezi kumpeleka kwa matibabu, akakopa pesa Agha Khan Hospital akaenda kutibiwa Ujerumani, aligundulika kuwa  ana saratani ambayo alikaa nayo na kuja kufariki miaka kumi baadae akiwahudumia Watanzania Muhimbili, akufundisha Madakari wa upasuaji, alifariki na kuzikwa hatukuona wala salamu toka kwa Rais!
4.Tuna wiki tatu sasa amefariki Dkt. Bashiri aliyekuwa daktari mzuri sanakwa vipimo vya ultrasound, amehudumia Watanzania wengi, sijasikia Rais anahudhuria.


Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini wanasema
Hivi...

.Huwa anachagua vipi misiba ya kuhudhuria?
.Hao washauri wake wanatoka katika kundi lipi  katika  jamii?
Source jf
 

 

No comments:

Post a Comment