Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Monday, February 4, 2013

"Midoli" ya watawala wa kiafrika katika picha.

Juma lililopita, Tanzania ilipokea ugeni kutoka Democratic Repubic of Congo uliokuwa ukiongozwa na Rais Laurent Kabila. Bila shaka kama ilivyo desturi ya ujio kama huo, ulikuwa ni wa kitaifa. Ujio huo unadhihirisha ni jinsi gani viongozi wa Afrika walivyokua mbali ya uhalisia [out of touch with reality]. 

Viongozi wengi hujinadi juu ya ufahamu wao wa hali ngumu ya kimaisha barani na hupenda wafahamike kama watu ambao wapo kwa ajili ya maslahi ya watu masikini ambao ndio wachaguzi wao. Kwa mtizamo wa karibu zaidi, mtu huweza kubani kuwa wengi wao kama si wote ni waongo [simply liars]. Huwezi kushuhudia juhudi za dhati za kutaka kuwakomboa watu wao kimaisha miongoni mwa viongozi hawa. Tizama vipaumbele vyao.

Katika hali ya kawaida, tungetaraji kuona viongozi wa bara la Afrika wakiwa wapole [humble] ili kuelezea aina ya maisha wanayoishi watu wao. Hata hivyo ni tofauti. Wanafundisha maji na kunywa mvinyo. Hii hujidhihirisha kupitia maisha ya anasa na undumilakuwili [hypocrisy] ambayo watawala hawa wanakuwa wamejichagulia. Pichani, ni baadhi tu ya 'midoli' ya watawala wa kiafrika.

Hiki ni 'kibajaji' cha 'mtukufu' sana [kama wasemavyo wenyewe] J.M Kikwete

Dala dala ya Raisi Lurent Kabira wa DRC alias Zaire.

Mjengo wa Raisi Jacob Zuma ambao uligharimu dola za kimarekani 25 milioni kuwa katika hali hii. Kule soweto vipi? Mbona watu wake wanaishi kwenye mabati?
Uwaziri Tanzania huambatana na "pipi" kama hizi.

Raisi Yoweri Museveni hataki shida.

Haya ndiyo mazingira halisi ya wapigiwa kula. Heaven on earth. Mh Getrude Rwakatare kweli anawakilisha. Ni lini mtu huyu atatambua madhila ya watu wake?

Wabunge wa Tanania hawataki shida. Hili ndilo jengo la bunge litumikalo kwa msimu. What a waste.

Maisha mazuuri kabisa. Msafara wa Raisi Goodluck Jonathan wa Nigeria na ulinzi mkali.


IN CONTRAST


Wapi uhuru wa kujieleza na usawa mbele ya sheria? Dr. Ulimboka mara baada ya kuwekewa 'make up'

Hizi ndizo shule za walala hoi. Atakuwa na mchango gani huyu katika taifa? Bila shaka kazi za sulubu zitamfaa.

Mauaji ya wachimba madini kule Afrika kusini mwaka jana. Wapi Zuma?


Njaa kali


Haya ndiyo maisha halisi ya wapiga kura wengi.

Ukame. Huyu naye ni mpiga kura. Kura yake imemsaidiaje?

Kilele cha utawala mbovu, ukiukwaji wa haki za binadamu na ukosefu wa uwajibikaji. Daudi Mwangosi aliuawa kikatili na Polisi wa kitanzania.

WHO CARES?

No comments:

Post a Comment