Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Monday, May 20, 2013

MACHINGA WAPIGWA MABOMU,RAIA WENGINE WAATHIRIKA,MMOJA ARARULIWA PAJI LA USO

Hivi ndivyo ilivyokuwa jana katika eneo la mashine tatu baada ya serikali kukataa kusikiliza malalamiko ya machinga juu ya namna ya uendeshwaji wa mnada siku ya jumapila katika eneo hilo


Ikumbukwe kuwa hiki ni kilio cha muda mrefu cha wamachinga kutafutiwa eneo zuri na lililoandaliwa kitaalam   kwa ajili ya shughuli zao kabla ya kuwaondoa mahali hapo ambapo ndipo chakula chao kinapopatikana

Machinga hao baada ya kuona serikali haisikilizi kilio cha waliamua kurudi eneo hilo bila kibali cha manispaa na ndipo jeshi  la polisi lilipotumwa kwenda kuwaondoa kwa nguvu.

Mbunge wa jimbo hilo Mhe Peter Msigwa ambaye alionekana kupita eneo hilo ameitwa kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano na mpaka naingia mtandaoni sikuwa na taarifa zozote za kuachiwa.

Abiria na wapiga debe stendi kuu wakinawa maji baada ya
 kupigwa mabomu na kumwagiwa maji ya kuwasha na askari wa FFU hapo jana



Hali ikiendelea kuwa tete kwa machinga kufunga barabara kuu ya Iringa Dodoma na ile ya mashine tatu


wananchi wakishaanga matairi yaliyochomwa barabarani na watu wenye hasira kali

















mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwasili eneo la vurugu kabla ya kuanza kwa vurugu hizo
Mbunge Msigwa akiondoka eneo la mashine tatu
Machinga wakisukuma gari ya mbunge Msigwa
Polisi wakimfuatilia mbunge Msigwa kwa nyuma baada ya kufika eneo hilo bila kufanya biashara kama alivyoahidi
Polisi wakianza kufukuza wananchi eneo

No comments:

Post a Comment