Edwin Bliss C

Success does not mean the absence of failure; it means the attainment of ultimate objectves. It means winning the war, not every battle.

Kufanikiwa hakumaanishi kushinda kila jambo; kunamaanisha kufikia malengo. Kunamaanisha kushinda vita na sio kila pambano.

Monday, May 20, 2013

NGUVU YA UMMA YASHINDA UCHAGUZI CHUO KIKUU CHA RUCO

Kwanza namshukuru MUNGU wa mbinguni kwa kuwa mwaminifu kwetu tangu wakati wa kuanza mchakato wa uchaguzi hadi kupatikana kwa ushindi.

Lakini pia niwashukuru wanafunzi wote waliotupigia kura na wasiotupigia kwa maombi yao ya usiku na mchana hadi tumeibuka kidedea katika uchaguzi huo ambao ulikuwa ni wa kihistoria

Haikuwa kazi rahisi kama inavyoweza kudhaniwa bali ilikuwa ni safari iliyojaa fitina,majungu,unafiki huku ikitawaliwa na wimbi kuu la USALITI.

Wenzetu wengi walijitenga nasi huku wakiinua vikwazo mbalimbali, wengine walisema tunatembea na bendera za vyama,wengine wakasema tumetumia mavazi ya chama, na hata wengine wakadiriki kusema kuna kiongozi mkubwa wa chama alishiriki nasi kupanga namna ya kumpata Rais.

Lakini sisi tunakiri kwamba kama si NGUVU YA UMMA, iliyotuamini na kutusikiliza na hatimaye kutupa ridhaa sisi hatukuwa chochote katikati ya wana wa RUCO,yote yaliyosemwa na fitina zote zilizofanywa ilikuwa ni mpango wa makusudi kabisa wa watu fulani kutugawa sisi watoto wa baba mmoja.

Leo tarehe 20/05/2013 mnamo saa 8:16 za usiku alitangazwa bwana MSANGI RUSTON kuwa Rais halali wa chuo kikuu cha RUCO na Bi FLORAH YOHANA kuwa makamo wa Rais kwa mwaka wa masomo 2013/2014

Ikumbukwe kuwa mwaka jana wakati wa uchaguzi vurugu kubwa zilitokea baada ya Mkuu wa Mkoa kutoa vitisho kwa baadhi ya wajumbe wa tume na wengine kupewa amri ya kujitoa ili wampitishe mgombea ambaye lilikuwa chaguo lake




SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU
Edit / Delete

No comments:

Post a Comment